24/05/2025
Kupitia kwenye kipindi chake cha Recap, ameizungumzia ep mpya ya Juma Jux ya A DAY TO REMEMBER aliyoitoa jana.
Anasema kwa sasa Jux ameaanza ku-set Standard ya muziki wake ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, ameanza kuwa na quality kubwa ya muziki.
Anaongeza Ukweli ni kwamba kwa sasa Jux ni mkubwa nje ya Tanzania kwa sababu ndani ya Tanzania wengi bado hawaamini na wanamu-Underrete.
Kwa sasa Jux kwenye mtandao wa Spotify ameshika nafasi ya pili Tanzania baada ya Diamond, Afrika Mashariki nafasi ya nne.
Monthly Listener ya Jux Spotify ni 853k ambapo Diamond ana milioni 1.5, Harmonize ana 583k na Rayvanny 466k Spotify, Alikiba ana 229k na Marioo 500k
Miezi mitano iliyopita Jux hakuwepo Top 5 Tanzania na hakuwepo Top 10 Afrika Mashariki, leo Tanzania nafasi ya pili na Afrika Mashariki nafasi ya nne.
Nafasi ya kwanza Afrika Mashariki ni.
1. Sofia nzau wa Kenya milioni 9
2. Diamond Tanzania milioni 1.5
3. Idd Aziz Kenya milioni 1.1
4. jux Tanzania 853k
5. Bien Kenya 803
Kwa speed hii na baada ya kuachia EP JUX atafikia milioni 1 muda sio mrefu.
Unakubaliana naye ✍🏿